Hardcover

Jamhuri ya Plato: Tafsiri ya Julius Nyerere

by Julius Kambarage Nyerere

Original price was: Sh 80,000.Current price is: Sh 75,000.

FREE Delivery for orders above Tsh 100k within Tanzania. T & C Apply.

Standard Delivery (Tsh 2,000 - Tsh 10,000) depending on your location.

Book picture is for illustrative purposes only, actual binding, cover or edition may vary.

Jamhuri ya Plato: Tafsiri ya Julius Nyerere

Jamhuri ni tafsiri pekee ya Kiswahili ya kitabu maarufu, The Republic, cha Plato iliyofanywa na Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Tafsiri hii inayochapishwa kwa mara ya kwanza miaka 25 baada ya kifo cha Nyerere, inatoa mwangaza wa kina juu ya maono yake kuhusu jamii na uongozi. Katika tafsiri hii, Mwalimu anawasilisha mawazo ya Plato kuhusu jamii bora, na haki, huku akiakisi maono yake binafsi kuhusu uongozi na mustakabali wa taifa. Jamhuri itakupeleka katika safari ya fikra, ambapo Sokrates na wenzake wanachambua haki, mifumo ya utawala, na nafasi ya elimu katika kujenga jamii iliyo bora. Kwa kutumia hadithi ya jamii inayotawaliwa na viongozi wenye hekima, Plato anasisitiza umuhimu wa maarifa, maadili, na usawa. Tafsiri hii ya Mwalimu Nyerere inachochea mjadala wa haki, utawala bora, na maadili katika dunia ya leo. Ni mwaliko wa kuchunguza upya mifumo yetu ya kijamii na kisiasa kwa mtazamo mpya na wa matumaini. Hiki ndicho kitabu cha mwisho cha Mwalimu Nyerere na urithi wake wa mawazo kwa vizazi vijavyo. Haya sasa kazi kwako! Kinunue, kisome, na kihifadhi ili kiwe urithi kwa kizazi chako pia.

Jamhuri ya Plato: Tafsiri ya Julius Nyerere

Jamhuri ni tafsiri pekee ya Kiswahili ya kitabu maarufu, The Republic, cha Plato iliyofanywa na Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Tafsiri hii inayochapishwa kwa mara ya kwanza miaka 25 baada ya kifo cha Nyerere, inatoa mwangaza wa kina juu ya maono yake kuhusu jamii na uongozi. Katika tafsiri hii, Mwalimu anawasilisha mawazo ya Plato kuhusu jamii bora, na haki, huku akiakisi maono yake binafsi kuhusu uongozi na mustakabali wa taifa. Jamhuri itakupeleka katika safari ya fikra, ambapo Sokrates na wenzake wanachambua haki, mifumo ya utawala, na nafasi ya elimu katika kujenga jamii iliyo bora. Kwa kutumia hadithi ya jamii inayotawaliwa na viongozi wenye hekima, Plato anasisitiza umuhimu wa maarifa, maadili, na usawa. Tafsiri hii ya Mwalimu Nyerere inachochea mjadala wa haki, utawala bora, na maadili katika dunia ya leo. Ni mwaliko wa kuchunguza upya mifumo yetu ya kijamii na kisiasa kwa mtazamo mpya na wa matumaini. Hiki ndicho kitabu cha mwisho cha Mwalimu Nyerere na urithi wake wa mawazo kwa vizazi vijavyo. Haya sasa kazi kwako! Kinunue, kisome, na kihifadhi ili kiwe urithi kwa kizazi chako pia.

Customers Who Bought This Item Also Bought ...